Breaking

Thursday, 26 February 2026

MBUSULE BOY AINGIA RASMI KWENYE RAMANI YA BONGO NA “MAJI YA MOTO”

 


Msanii chipukizi anayekuja kwa kasi kwenye muziki wa Bongo, Mbusule Boy, jina lake halisi Kelvin Juma, ametambulisha rasmi wimbo wake mpya unaoitwa “Maji ya Moto.” 

Ametokea Mwanza na kwa sasa anaishi Dar es Salaam ambako anaendelea kukuza kipaji chake cha muziki kwa bidii.

Mbusule Boy yupo chini ya lebo ya Bank Boys Record inayomilikiwa na Don Cash, ambaye pia ni meneja wake. 

Kupitia usimamizi huo, tayari ameachia jumla ya nyimbo sita zinazopatikana kwenye majukwaa yote ya kidijitali.

Mbali na “Maji ya Moto,” nyimbo zake nyingine ni pamoja na Uzuri Wako, Katoto, Nasikia Raha, Unaniumiza na Mimi na Wewe. 

Wimbo wa “Maji ya Moto” umetolewa Februari 2026, ukiwa umetayarishwa na Mbusuleba huku mtunzi na mtayarishaji wa mashairi akiwa ni Kelvin Juma mwenyewe.

Msanii huyo amesema muziki kwake ni maisha na pia ni biashara, na amewaomba Watanzania kumpokea na kumshika mkono katika kila hatua ya safari yake ya muziki, akiahidi kuendelea kutoa kazi bora zenye ubunifu na mvuto wa kipekee.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: +255 621 896 990

Pages