Breaking

Friday, 18 July 2025

BODI YA ITHIBATI YAWAPIGA MARUFUKU WATANGAZAJI WANNE MJINI FM KUJIHUSISHA NA MASUALA YA KIHABARI

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imewapiga marufuku watangazaji wa kituo cha redio cha Mjini FM kujihusisha na kazi za kihabari kuanzia Julai 18, 2025, kufuatia ukiukwaji wa Sheria na maadili ya taaluma ya habari.

Kwa mujibu wa taarifa ya Bodi hiyo, adhabu hiyo inawahusu watangazaji Deodatha William, Mussa Crispin Mgenge, Perfect Crispin na Iddy Bakari Iddy waliokuwa wakirusha kipindi mubashara kiitwacho GENGE LA GEN TOK, kilichofanyika Julai 16, 2025  ambapo walifanya mahojiano na msanii wa Singeli aitwaye Dogo PATEN.



Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: +255 621 896 990

Pages