
Serikali imetangaza kulifutia usajili Kanisa la Ufufuo na Uzima, linalomilikiwa na Mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima, ikiwa ni siku moja tangu kiongozi huyo wa kiroho atangaze msimamo wake wa kuendelea kukemea vitendo vya utekaji na watu kupotea.
Sababu ya uamuzi huo wa Msajili wa Jumuiya za Kiraia, Emmanuel Kihampa ni kile kilichoelezwa, kanisa hilo limekiuka Sheria ya Jumuiya Sura ya 337, kwa kutoa mahubiri yenye mwelekeo wa kisiasa na nia ya kuichonganisha Serikali na wananchi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo, Jumatatu Juni 2, 2025 na Kihampa, kitendo kilichofanywa na Askofu Gwajima kinaweza kuhatarisha amani na utulivu nchini.
Soma zaidi HAPA