; //]]>
  • Home
  • About
  • Contact

LANGO LA HABARI
    • HABARI
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MATUKIO
    • MAGAZETI
    • MADINI
    • MICHEZO
    • BURUDANI
    • MAKALA
  • Breaking

    Thursday, 24 March 2022

    Home HABARI KITAIFA WAZIRI BITEKO AZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI WIZARA YA MADINI, AWATAKA KUJIEPUSHA NA VITENDO VYA RUSHWA

    WAZIRI BITEKO AZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI WIZARA YA MADINI, AWATAKA KUJIEPUSHA NA VITENDO VYA RUSHWA

    Lango la Habari March 24, 2022 ,HABARI ,KITAIFA




    WAZIRI wa Madini, Dkt.Doto Biteko amezindua Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Madini huku akiwapongeza kwa namna ambavyo wanafanya kazi kwa ufanisi, hivyo kuwezesha mafanikio chanya nchini.


    Waziri Dkt. Biteko amezindua baraza hilo jana jumatano Machi 23, 2022 mkoani Morogoro huku akirejea wito wake wa mara kwa mara kwa watumishi kuwa, wanapaswa kufanya kazi kwa uadilifu na kuepuka vitendo vya rushwa.

    Amesema, Sekta ya Madini ni moja ya sekta ambayo inatakuwa kuwa makini na vitendo vya rushwa kwani inadhoofisha utoaji huduma na kuondoa haki kwa wananchi.

    "Wizara haitamvumilia mtumishi yoyote atakayebainika na kuthibitika kujihusisha na vitendo vya rushwa. Hakikisheni mnabeba dhamana hii na kutekeleza kikamilifu wajibu wenu kwa weledi na kwa kuzingatia maadili ya kitaaluma na ya utumishi wa umma,"amesema Waziri Dkt Biteko


    Aidha amewaasa kujadili namna ya kuimarisha ustawi wa wafanyakazi na kujifanyia tathmini kuelekea miaka mitano tangu kuanzishwa kwa wizara hiyo.


    "Nendeni mkawakumbushe watumishi mnaowaongoza hivi karibuni wizara inatimiza miaka 5 tangu kuanzishwa kwake, jifanyieni tathmini msibweteke na mafanikio yaliyopatikana, angalieni viashiria hatarishi mvifanyie kazi msirudi nyuma" amesema



    Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adolf Ndunguru amsema kuwa, umoja, mshikamano na bidii za watumishi hao zimewezesha kukusanya Shilingi Bilioni 406 kuanzia Julai 2021 hadi Februari 2022.


    Amesema mchango wa Sekta ya Madini kwenye Pato la Taifa umeendelea kuimarika. 

    "Katika kipindi hiki mchango wa Sekta ya Madini kwenye Pato la Taifa umendelea kuimarika ambapo katika kipindi cha miezi tisa (Januari hadi Septemba 2021) mchango wa Sekta ya Madini kwenye Pato la taifa uliongezeka hadi kufikia asilimia 7.3 kutoka mchango wa asilimia 6.5 katika kipindi kama hicho kwa mwaka 2020.



    "Katika robo ya Tatu Julai- Septemba 2021, Sekta ya Madini imechangia asilimia 7.9 ya Pato la Taifa, Mwelekeo unaonesha kuwa malengo yetu ya kuhakikisha sekta hii inachangia asilimia 10 ya Pato la Taifa ifikapo mwaka 2025 kama ilivyo matakwa ya Dira ya Taifa ya Maendeleo, 2025 na Mpango wa tatu wa Maendeleo ya Taifa yanatekelezeka kila mtu akitimiza wajibu wake.


    "Katika kipindi cha kuanzia Julai 2021 hadi kufikia Februari 2022, tumefanikiwa kukusanya maduhuli ya shilingi bilioni 404.6, sawa na asilimia 62.6 ya lengo la makusanyo.


    Amefafanua kuwa, kupitia STAMICO imewezesha mafunzo na huduma mbalimbali kwa wachimbaji wadogo wapatao 1,144 waliotembelea vituo vya mfano vya Katente, Lwamgasa na Itumbi.


    "Tumendelea kutangaza fursa zilizopo katika Sekta ya Madini kupitia mikutano ya kitaifa, kikanda na kimataifa ukiwemo mkutano wa kimataifa tulioandaa mwezi februari 2022. Tumeboresha Sheria, Kanuni na Miongozo mbalimbali kwa lengo la kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji.


    Pamoja na mafanikio Katibu Ndungulu amesema wizara hiyo inakabiliwa na changamoto za uwepo wa shughuli za utoroshaji wa madini zinazosababisha upotevu wa mapato ya serikali, uelewa mdogo wa wachimbaji, wafanya biashara wa madini na umma kwa ujumla kuhusu Sheria ya madini, hivyo kusababisha uwepo wa migogoro ya mara kwa mara.


    "ili kukabiliana na changamoto hizo,amesema wizara imeweka mikakati na hatua mbalimbali ya kukabiliana nazo ikiwemo kuimarisha usimamizi wa shughuli za madini na ukusanyaji wa mapato ya serikali yatokanayo na wasilimali madini kwa kushirikisha mamlaka mbalimbali." Ameeleza 




    Naye Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Wizara ya Madini, Joseph Ngulumwa amesema kuwa, wanaushukuru uongozi wa wizara kwa namna ambavyo wamekuwa wakiwezesha watumishi kuhudhuria mafunzo mbalimbali.


    "TUGHE tunatoa shukrani za dhati kwa uongozi wa wizara kwa kuendelea kuwezesha watumishi kuhudhuria mafunzo ya muda mrefu na mfupi kwani mafunzo haya yanasaidia kuongeza weledi na ufanisi katika kazi za wizara."Katika kuongeza uwezo wa watumishi, tunashauri watumishi kupatiwa uzoefu katika nchi zilizoendelea katika shughuli za uchimbaji madini na utafiti wa madini kama Australia, Canada na mataifa mengine yaliyoendelea. Aidha, tunashauri kuweka bajeti ya kusomesha wataalam nje ya nchi katika Shahada za Uzamili na Uzamivu walau watumishi 5 kwa mwaka.


    "TUGHE inatambua kuwa michezo ni sehemu ya kuboresha afya kwa watumishi hivyo, Uongozi wa TUGHE unashauri wizara kuwezesha watumishi kushiriki michezo mbalimbali mfano SHIMIWI na BONANZA kwa kuwa na bajeti ya kutosha na kushiriki vema.
    "Kwa niaba ya wafanyakazi, tunaomba suala la wafanyakazi bora kuongeza idadi kutoka mtumishi mmoja kuwa watumishi wawili kwa kila Idara na Kitengo ili kupanua wigo wa motisha kwa watumishi,"amesema Mwenyekiti huyo.










    TAZAMA MATUKIO YA PICHA HAPA CHINI
























    Tags HABARI# KITAIFA#
    Share This
    Author Image

    About Lango la Habari

    KITAIFA
    by Lango la Habari - March 24, 2022
    Tags HABARI, KITAIFA
    Newer Post Older Post Home
    Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: +255 621 896 990
    Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

    LANGO LA HABARI TV

    ZILIZOKIKI WIKI HII

    • SERIKALI YAKABIDHI VITENDEA KAZI KUBORESHA HUDUMA ZA UMEME TANESCO SHINYANGA
      SERIKALI YAKABIDHI VITENDEA KAZI KUBORESHA HUDUMA ZA UMEME TANESCO SHINYANGA
          Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, akijaribu kuendesha moja ya magari yaliyokabidhiwa kwa TANESCO Mkoa wa Shinyanga, wakati w...
    • SEKTA YA MAZIWA YAPATA NGUVU MPYA: WAKAGUZI WAPEWA MAFUNZO MOROGORO
      SEKTA YA MAZIWA YAPATA NGUVU MPYA: WAKAGUZI WAPEWA MAFUNZO MOROGORO
      Sekta ya maziwa nchini imepata msukumo mpya kufuatia kuanza kwa mafunzo maalum kwa wakaguzi wa maziwa kutoka mikoa ya Morogoro, Kilimanjaro,...
    • WATUMISHI WA TEA WAAGIZWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA UFANISI.
      WATUMISHI WA TEA WAAGIZWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA UFANISI.
      Dkt. Edith Rwiza Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia akiongea na Wajumbe wa ...
    • RABIA AAGIZA WAKALIMANI WA LUGHA ZA ALAMA KWENYE OFISI ZA UMMA
      RABIA AAGIZA WAKALIMANI WA LUGHA ZA ALAMA KWENYE OFISI ZA UMMA
           Katibu wa NEC, siasa na uhusiano wa kitaifa (SUKI) Rabia Abdallah Hamid akizungumza. Na Marco Maduhu, SHINYANGA Katibu wa NEC, Siasa na...
    • ELIMU YA KUMLINDA MLAJI YATOLEWA KATIKA SHULE YA SEKONDARI MNAZI MMOJA
      Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi kutoka FCC, Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mm...
    • ORYX GAS YAENDELEA KUSOGEZA NISHATI SAFI KWA WANANCHI KWA KUZINDUA DUKA WILAYANI CHATO,EWURA YATOA NENO
      ORYX GAS YAENDELEA KUSOGEZA NISHATI SAFI KWA WANANCHI KWA KUZINDUA DUKA WILAYANI CHATO,EWURA YATOA NENO
      Wananchi wa Wilaya ya Chato mkoani Geita wamepata fursa ya kupata nishati safi ya kupikia kwa urahisi zaidi kufuatia uzinduzi wa duka jipya ...
    • Wadau waaswa kuwekeza katika matumizi ya teknolojia kuchakata taka
      Wadau waaswa kuwekeza katika matumizi ya teknolojia kuchakata taka
      Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamadi Yussuf Masauniakizungumza na wananchi katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya...
    • OFISI YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI YAWAJENGEA UWEZO WATAALAM WA TIBA ASILI
      OFISI YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI YAWAJENGEA UWEZO WATAALAM WA TIBA ASILI
      Mkuu wa wilaya ya Ukerewe, Mhe. Christopher Ngubiagai (aliyesimama),akizungumza wakati akifungua mafunzo kwa waganga wa tiba asili na tibamb...
    • NEMC YAHAMASISHA UBUNIFU WA BIDHAA ZITOKANAZO NA TAKA
      NEMC YAHAMASISHA UBUNIFU WA BIDHAA ZITOKANAZO NA TAKA
      NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa...
    • Italia Yaadhimisha Siku ya 10 ya Ubunifu Duniani
      Italia Yaadhimisha Siku ya 10 ya Ubunifu Duniani
      Balozi wa Italia nchini Tanzania, Giuseppe Sean Coppola, amesema kuwa Italia inaadhimisha toleo la 10 la Siku ya Ubunifu wa Italia Duniani, ...

    MICHEZO

    Categories

    BURUDANI HABARI HALI YA HEWA KITAIFA MAGAZETI MAHUSIANO

    Pages

    WASILIANA NASI

    Name

    Email *

    Message *

    KUHUSU SISI

    Lango la Habari ni tovuti inayojihusisha na usambazaji wa taarifa mbalimbali katika nyanja za kitaifa, kimataifa, biashara, michezo na burudani.

    Tags

    HABARI KITAIFA MAGAZETI MATUKIO MICHEZO DAWASA MADINI LIVE BURUDANI UTEUZI KIMATAIFA African Doctors BIASHARA ZOOM BRELA AJIRA MAHUSIANO MAKALA SIASA KENYA CHADEMA LOLIONDO MITIHANI SAMIR UKATILI TZ-MW MONKEYPOX TRENI haba HALI YA HEWA UTAMADUNI ANGA MAPENZI ki

    Send Quick Message

    Name

    Email *

    Message *

    Copyright © LANGO LA HABARI