Breaking

Wednesday, 16 March 2022

AKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUJIFANYA AFISA USALAMA WA TAIFA



Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja linamshikilia YUNUS NASSOR ALI (32) kwa tuhuma za kujifanya afisa usalama wa Taifa.


Akithibitisha tukio hilo mbele ya waandishi wa habari Kamanda wa polisi mkoa wa Mjini Magharibi ACP. ABDALLAH MUSSA amesema mtuhumiwa huyo alikamatwa mnamo tarehe Machi 11, 2022 majira ya saa 11:00 jioni  huko Kilima Hewa wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi ambapo alihusika katika matukio mbalimbali ya wizi wa pikipiki aina ya Click pamoja na kujifanya Afisa Usalama wa Taifa.



Aidha baada ya kufanya upekuzi nyumbani kwake Kilima Hewa Wilaya ya Mjini alipatikana na nyaraka mbalimbali za Serikali.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: +255 621 896 990

Pages